MigogoroUkraine
Rais Trump akutana na Zelensky na kufanya mazungumzo
26 Aprili 2025Matangazo
Mkurugenzi wa mawasiliano wa White House Steven Cheung amesema kwamba wakuu hao wawili wamekutana kwa faragha leo na wamekuwa na majadiliano yenye tija sana.
Hata hivyo hakutoa maelezo zaidi, akisema tu kwamba yatafuata baadae.
Viongozi hao hawajakutana ana kwa ana tangu walipolumbana kwenye kwenye ofisi ya Oval huko White House mnamo mwezi Februari.
Trump anashinikiza kupatikana kwa makubaliano ya amani nchini Ukraine na jana Ijumaa alisema wanakaribia kuafikiana baada ya mazungumzo kati ya mjumbe maalumu wa Marekani Steve Witkoff na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Moscow.