SiasaUfaransa
Macron azungumza na Erdogan kuhusu hali inayoendelea Syria
8 Februari 2025Matangazo
Macron amesisitiza juu ya umuhimu wa kuheshimu kipindi cha utawala wa mpito, umoja na uhuru wa taifa hilo la Syria , pamoja na haja ya kuendeleza mapambano dhidi ya kundi la kigaidi linalijiita Dola la Kiislamu IS.
Aidha, Rais Erdogan amepongeza hatua ya Umoja wa Ulaya kuanza kulegeza vikwazo dhidi ya Syria na amemueleza Macron kuwa ulikuwa uamuzi sahihi lakini akasisitiza kuwa vikwazo hivyo vinapaswa kuondolewa kabisa kwa manufaa ya uongozi mpya.