SiasaMarekani
Rais Donald Trump kumteua Waltz kuwa balozi kwenye UN
2 Mei 2025Matangazo
Trump ametoa tangazo hilo kupitia mtandao wake wa kijamii, wa Truth Social na Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio atashika nafasi hiyo kwa muda.
Tangazo hilo lilitolewa saa chache kufuatia ripoti kwamba Waltz na naibu wake, Alex Wong, watajiuzulu nafasi zao, wakati shinikizo likizidi kuhusu jukumu la Waltz kwenye kashfa ya Signalgate.
Waltz alimuunga bila kukusudia mwandishi wa habari kwenye kundi ambalo hujadiliana taarifa za siri hususan za mipango ya vita, hatua iliyobua madai ya taarifa hizo kuvuja.