SiasaHaiti
Genge lenye silaha lawafungulia wafungwa 500 Haiti
1 Aprili 2025Matangazo
Msemaji wa polisi, Lionel Lazzare, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba sasa wametwaa udhibiti wa mji wa Mirebalais, ulio umbali wa kilomita 55 magharibi mwa mpaka wa Haiti na Jamhuri ya Dominiki. Ripoti za awali zinasema genge hilo lenye silaha kwa jina la Viv Ansanm, lilivamia gereza na kukichoma moto kituo kimoja cha polisi cha mji huo.
Taifa hilo la Karibiani limekumbwa na machafuko ya magenge kwa miaka kadhaa na juhudi za kimataifa kuleta utulivu zimegonga mwamba hadi sasa.