JamiiUturuki
Watu 30 wakamatwa Istanbul kwa kushiriki sherehe za mashoga
29 Juni 2025Matangazo
Hayo yameelezwa na mwanasiasa wa upinzani Kezban Konukcu, ambaye pia ni mbunge kutoka Chama cha DEM kinachounga mkono jamii ya Wakurdi.
Picha na video kutoka shirika la habari la Reuters zimeonyesha polisi wakigombana na kundi la wanaharakati waliokuwa na bendera za rangi ya upinde wa mvua zinazowatambulisha mashoga kabla ya kuwakusanya na kuwapakia kwenye magari ya polisi.
Kwa miaka mingi Uturuki imekuwa ikizuia matukio yoyote yanayohusisha jamii ya mashoga na mashirika kadhaa ya kutetea haki za binaadamu yamekuwa yakilaani hatua hizo.