MigogoroUbelgiji
Polisi waimarisha ulinzi kabla ya mkutano wa wakuu wa Ulaya
6 Machi 2025Matangazo
Mkutano huo unafanyika baada ya hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuifutia msaada wa kijeshi Kiev na kuongeza wasiwasi, kwamba bara hilo haliwezi tena kutegemea ulinzi wa Marekani.
Akiwasili kwenye mkutano huo, Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani ametowa tahadhari kuhusiana na fikra ya kutumika silaha za Nyuklia za Ufaransa kuyalinda mataifa mengine ya Ulaya.
Viongozi wa nchi 27 wanachama wa Umoja huo watashiriki mkutano huo pamoja na Rais Volodymyr Zelensky. Hata hivyo, mshikamano wa mataifa hayo kwa Ukraine, huenda ukagubikwa na hatua ya Hungary ya kukataa kuidhinisha tamko la kuiunga mkono Kiev.