JamiiSri Lanka
Polisi wa Sri Lanka wachunguza vifo vya watalii wawili
8 Februari 2025Matangazo
Watalii hao, ambao ni wanawake, mmoja akiwa raia wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 na Mjerumani mwenye umri wa miaka 26, walikutwa wakiwa mahtuti katika vyumba vyao vya kulala wageni katika mji mkuu Colombo na walifariki baadaye baada ya kupelekwa hospitali. Mwanaume mmoja raia wa Ujerumani bado anapatiwa matibabu hospitalini.
Vyombo vya habari vya Sri Lanka viliripoti kuwa kabla ya tukio hilo, vyumba vya hosteli hiyo vilipuliziwa dawa yenye sumu ili kutokomeza kunguni na wadudu wengine na kwamba kwa sasa imefungwa na polisi ili kupisha uchunguzi zaidi.