Polisi Ujerumani ina wasiwasi kuhusu waomba hifadhi
4 Juni 2025Matangazo
Katika kesi ya kwanza kuibuka kuhusu hatua hiyo tata, mahakama kuu ya Berlin ilitoa uamuzi siku ya Jumatatu unaowapa haki raia watatu wa Somalia waliorejeshwa Poland mnamo Mei 9, na kusema kwamba walipaswa kushughulikiwa chini ya Kanuni ya Dublin ya Umoja wa Ulaya kwa kesi za hifadhi.
Mamia waaandamana Berlin dhidi ya CDU kuhusu kura ya uhamiaji
Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, ametetea sera hiyo, lakini leo, mwenyekiti wa chama cha polisi, Andreas Rosskopf, amesema ana wasiwasi kuhusu athari za maamuzi ya mahakama kwa maafisa ambao wataendelea kuwarudisha watu mipakani.
Rosskopf amesema hatimaye maafisa wapolisi wanapaswa kuwajibika kwa matendo yao wenyewe.