Pica ni ugonjwa wa kitabia unaomfanya mtu kuwa na hamu ya kula vitu visivyo chakula na visivyo na thamani ya lishe, kama vile udongo, chokaa, sabuni, barafu, mchanga, karatasi au plastiki. Hali hii hutokea zaidi kwa watoto, wanawake wajawazito, na watu wenye matatizo ya akili au upungufu wa virutubisho mwilini kama chuma (iron) au zinki (zinc). Sikiliza makala hii ya Alex Mchomvu.