Papa Leo atoa ujumbe wa mazungumzo na umoja kwa Makadinali
24 Mei 2025Matangazo
Papa Leo amesema mkutano wake na maafisa hao ulikuwa fursa ya kutoa shukrani kwa kazi yote inayofanywa na wote wanauunda chombo hicho cha utawala wa kanisa kinachofahamika kama Roman Curia
Pia, Papa aliwahimiza maafisa hao wa kanisa katoliki kuwa wajenzi wa umoja na kujiweka katika viatu vya wengine na kuepuka chuki.
Mtangulizi wake, Hayati Papa Francis alikuwa na uhusiano mgumu mara kwa mara na uongozi huo wa kanisa katoliki (Curia) pamoja na maafisa wa Vatican, baada ya mwanzoni kabisa kuwalaumu kwa tamaa ya madaraka.